Wednesday, April 20, 2016

COMPUTER GUIDE "JIFUNZE MWENYEWE" SEHEMU YA 3

Namna ya kuwasha na kuzima kompyuta

1.  Namna ya kuwasha kompyuta (mwanzo)

2.  Namna ya kuwasha bila kuizima kabisa

3.  Namna ya kuzima kompyuta (mwisho)

Namna ya kuwasha kompyuta katika hatua ya mwanzo kabisa.
Baada ya kuiunganisha kompyuta yako kwenye umeme, kilichobaki ni kuiwasha sasa.
Mbele yako ukiwa umeketi kuielekea kompyuta yako, unakuwa unatizamana na kompyuta yako.


Hapo unaona kuna kitufe kimoja kwenye compyuta yako kama k
inavoonekana kwenye picha hapo juu hiki ni lazima uhakikishe kimewashwa ili kompyuta yako ifanye kazi.

Kuwasha upya Kompyuta yako
(Restarting your Computer)

Kuwasha upya: Hii hufanywa pale ambapo kompyuta yako inashindwa kufanya kazi vizuri au kukwama (stuck).
Mara nyingi huwa inashauriwa kuizima kompyuta na kuiwasha upya pale inapokua na tatizo kama hilo.