Wednesday, May 11, 2016

5 Things to consider when buying a computer... Mambo 5 Muhimu kabla ya kununua komyuta..

Huu ni mfululizo wa mambo chungu nzima ambayo utakutana nayo unapotaka kununua kompyuta mpya.

Kununua kompyuta si jambo rahisi. Kuna aina nyingi mno za kompyuta. Unapaswa kwa kweli kununua kompyuta ambayo ni sahihi kwako ili usije kujuta baadaye.
Kwamba baada ya mwaka mmoja tu unajikuta haitoshelezi tena mahitaji yako.
Si kila kompyuta inatengenezwa sawa
Kompyuta hazitengenezwi kwa usawa. Na pia mahitaji ya mtu hayawezi kufanana na ya mwingine. Kwa hivyo manunuzi ya PC mpya yanategemeana na mahitaji yako.
Kama unataka kompyuta yenye uwezo mkubwa, itakubidi kulipa fedha nyingi zaidi. Katika muongozo huu, nitakuonesha ni kwa jinsi gani viungo vilivyo ndani ya kompyuta vina maana gani kwako.
Hii itakusaidia kuamua unahitaji nini na ni mambo yapi uyazingati zaidi.
Ni kwa jinsi hii ndiyo utaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kununua kompyuta inayokufaa na inayoendana na mahitaji yako. Utakuwa katika nafasi ya kuepuka kutumia fedha nyingi pasipo sababu.
Unataka Kompyuta Mpakato (Laptop) au ya Mezani (Desktop)?
Pengine huu ni uamuzi rahisi kwako.
Lakini pia ni uamuzi ambao utapelekea kuamua ni kiasi gani utatumia kununua kompyuta yako. Kwa sababu kama Laptop na Desktop zina uwezo unaolingana, laptop itakuwa aghali zaidi ya desktop.
Kwa nini?
Kwa sababu laptop ina sifa za ziada ambazo desktop haina. Laptop inaweza kubebwa mahali popote kwa sababu ina umbo dogo kuliko desktop. Laptop ni nyepesi zaidi ya desktop. Laptop ina betri ambayo inaiwezesha kutumika hata mahali pasipo na umeme.
 


Desktop                                                           Laptop                                                          
Kwa hivyo kama unataka kompyuta ambayo itatumika zaidi mahali pamoja bila haja ya kubebeka, nunua desktop. Desktop pia ina faida ya kwamba una uwezo wa kuitunza kwa uda mrefu zaidi ya laptop. kwa sababu ina nafas kubwa ya kupoza joto na hivyo kuwa na maisha marefu.
Pia ni rahisi kubadili au kuongeza vifaa katika desktop kuliko katika laptop. hii inakupa mwanya wa kuboresha kompyuta yako kutokana na mahitaji ya wakati husika hata kama umepita muda mrefu.
Kwa hivyo kama unahitaji kusafiri mara kwa mara, chagua laptop. Kumbuka pia kwamba kama mahitaji yako ni mambo madogo madogo kama vile kutuma na kupokea email au kutafuta taarifa mtandaoni, unaweza kununua kifaa cha mkononi (tablet) au hata laptop ndogo zaidi.
Lengo lako ni kusave fedha ambazo zitatumika katika shughuli nyingine.
Hasa katika kipindi hiki cha utumbuaji majipu.
Fahamu ubongo wa kompyuta unayotaka kununua
Ubongo?
Yeah.
Ubongo wa Kompyuta – CPU
Kompyuta ina ubongo ambao huendesha kila kitu, kama vile ubongo wako unavyokusimamia wewe. Ubongo wa kompyuta unaitwa processor, au central processing unit – CPU.
Kama unataka kompyuta yenye kasi, inayowashwa na kuwa tayari kwa haraka, na inayokamilisha kile unachoiambia kwa haraka, bila kuchelewa, basi nunua ile yenye CPU bora zaidi.
Utajuaje?
CPU hupimwa kwa kiwango cha Gigahertz – GHz. Kompyuta nyingi za siku hizi huwa zimebandikwa nembo inayoonesha uwezo wa CPU. Kadiri uwezo wa CPU unavyokuwa mkubwa ndiyo kiwango cha kuchakata taarifa kwa haraka kinavyoongezeka.


Picha hii utaiona ikiwa imebandikwa pembeni au ubavuni mwa kompyuta. Kompyuta nyingi siku hizi utaona zimebandikwa nembo zinazosema core i3, core i5, au core i7.
Core i7 maana yake CPU ina uwezo mkubwa zaidi kuliko core i5 na core i3. Hata hivyo kitaalam, kompyuta zenye core i3 zinatoa kelele hafifu kuliko zile zenye core i5 na core i7.
Uwezo wa nafasi ya kufanyia kazi (RAM)
Kiwango cha uwezo wa kuhifadhi taarifa na data wakati kompyuta ikifanya kazi kinaitwa RAM – Random access memory.
Ni kama vile tulinganishe chumba kidogo ambacho wanaishi watu 10 na uwanja wa mpira ambako watu 60,000 wanaweza kuenea kwa wakati mmoja.
Kadiri kompyuta inavyokuwa na RAM kubwa ndivyo inavyoongezeka uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Watu kumi watakaa kwa kujibana chumbani lakini ukiwachukua na kuwaweka katika uwanja, watajitanua watakavyo.

RAM ya Kompyuta
Nunua kompyuta yenye RAM kubwa zaidi. Kompyuta nyingi za kisasa zina RAM yenye Gigabyte 4 (4 GB) na kuendelea. Unapokuwa na kompyuta yenye RAM kubwa, unakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa haraka zaidi.
Kwa sababu kompyuta ina uwezo wa kushughulikia kazi nyingi kwa wakati mmoja.
Pia RAM zinatofautina, hata kama zote zina kiwango cha 4GB, kwa mfano. RAM yenye nembo DDR2-800 ina ufanisi mkubwa zaidi ya RAM yenye nembo ya DDR2-400.
Kadiri ukubwa wa RAM unavyoongezeka, ndivyo bei hupanda.
Uliza dukani kabla hujanunua.
Uwezo wa kutunza kumbukumbu (Hard Drive au Hard Disk)
Kila kompyuta inahitaji sehemu ya kutunza kumbukumbu – data storage. Sehemu hii ya kutunza kumbukumbu inaitwa hard disk au hard drive – kwa kifupi HDD.
Kompyuta nyingi siku hizi zinaanzia na HDD zenye ukubwa wa Gigabyte 500.
Unapochagua kompyuta, angalia mahitaji yako. Una mpango wa kuhifadhi data nyingi au kompyuta yako ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida tu? Hii itakusaidia kupunguza bei ya kompyuta kwani kwadri inavyokuwa na HDD kubwa ndivyo bei inavyoongezeka.

HARD DISK
EXTERNAL HDD
FLASH DISK


Kumbuka pia kuwa teknolojia imeendelea sana siku hizi. Kama huna fedha za kutosha lakini ungependea kuwa na sehemu kubwa zaidi ya kuhifadhi data, kuna vifaa vya ziada – peripheral devices.
Flash disks na External Hard Disk ni vifaa amnavyo unaweza kununua baadaye endpao mahitaji yako yataongezeka.
Angalia mahitaji au vifaa vya ziada – peripherals
Kuna vifaa gani vya ziada utavihitaji katika kompyuta yako? Unataka kompyuta yako uweze kufanya nini?
Hapa utatambua unahitaji vifaa vya ziada katika kompyuta yako kwa kutegemea utakavyoitumia kompyuta yako. Hebu tutazame baadhi ya mambo ya ziada:
Matundu ya USB – Universal Serial Bus (USB) slots.
Haya ni matundu kwa ajili ya kupachika vifaa muhimu katika kompyuta kama vile kipanya (mouse), keyboard, kipaza sauti, radio, na monitor. Matundu haya kwa hakika yanaweza kuunganisha kitu chochote cha kielektroniki.
USB Ports
Matundu ya USB